Advent Hymnals

170. JINA LANGU LIMEANDIKWA JE

Nyimbo Za Kristo,


1
Sitafuti mali, wala utajiri; Nataka kwa yakini nipate Mwokozi.
Chuoni mwa Ufalme, niambie Yesu, Jina langu yakini limeandikwa, je? 

Chorus
Limeandikwa, je? Jina langu huko? 
Kitabuni mbinguni, limeandikwa, je?

2
Dhambi zangu ni nyingi, ni kama mchanga, Lakini damu yako, Mwokozi, yatosha;
Kwani umeahidi: zijapo nyekundu Zitakuwa nyeupe ilivyo theluji. 

3
Mji mzuri sana, wa majumba makuu, Walipo malaika, mji bila ovu;
Wakaapo walio na mavazi safi, Limeandikwa sasa, jina langu huko? 

  • -
    Title Jina Langu Limeandikwa Je
    Key
    Titles undefined
    First Line Sitafuti mali, wala utajiri; Nataka kwa yakini nipate Mwokozi.
    Author
    Year
    Composer
    Hymnal -
    Tune
    Metrical pattern
    # Stanzas
    Chorus
    Chorus Type
    Subjects
    Texts
    Print Texts
    Scripture Song