Advent Hymnals

137. SAA HERI YA SALA

Nyimbo Za Kristo,


1
Saa heri ya sala tunapojidhili,
Kama tukija kwake Yesu rafiki;
Tukiwa na imani kwamba yu mlinzi, 
Waliochoka sana watapata raha.

Chorus
Saa ya sala, iliyo heri; 
Waliochoka sana watapata raha.

2
Saa heri ya sala, ajapo Mwokozi, 
Ili awasikie watoto wake.
Hutwambia tuweke miguuni pake 
Mizigo yetu yote: tutapata raha. 

3
Saa heri ya sala, wawezapo kuja Kwa Bwana
Yesu wanaojaribiwa; 
Moyo wake mpole, atawarehemu; 
Waliochoka sana watapata raha.

4
Saa heri ya sala tutakapopewa,
Mibaraka ya roho, tukimwamini; 
Kwa kuamini kweli hatutaogopa;
Waliochoka sana watapata raha.


  • -
    Title Saa Heri Ya Sala
    Key
    Titles undefined
    First Line Saa heri ya sala tunapojidhili,
    Author
    Year
    Composer
    Hymnal -
    Tune
    Metrical pattern
    # Stanzas
    Chorus
    Chorus Type
    Subjects
    Texts
    Print Texts
    Scripture Song