Advent Hymnals

132. BWANA NI MCHUNGA

Nyimbo Za Kristo,


1
Bwana ni Mchunga, Sitahitaji;
Majani mabichi malisho yangu.
Ananinywesha maji matulivu;
Atanirudisha nikipotea. 

2
Nipitapo bondeni mwa mauti 
U mlinzi wangu sitaogopa;
Fimbo lako latosha kunilinda;
Ukinifariji sina hasara. 

3
Kati ya mateso meza waandaa,
Na kikombe changu kinafurika;
Umenipaka kichwani mafuta;
Nitaulizaje zaidi kwako? 

4
Wema na fadhili zinifuate 
Siku zangu zote hata milele; 
Nami nitakaa nyumbani mwa Bwana 
Katika ufalme wa pendo lake.



  • -
    Title Bwana Ni Mchunga
    Key
    Titles undefined
    First Line Bwana ni Mchunga, Sitahitaji;
    Author
    Year
    Composer
    Hymnal -
    Tune
    Metrical pattern
    # Stanzas
    Chorus
    Chorus Type
    Subjects
    Texts
    Print Texts
    Scripture Song