Advent Hymnals
118. NILIPOTOKA KABISA
Nyimbo Za Kristo,
1
Nilipotoka kabisa, sasa narudi;
Nikakawia dhambini, Bwana narudi.
Chorus
Narudi nyumbani: daima kwako.
Kwa upendo nipokee: Naja nyumbani.
2
Nikasusurika sana, sasa narudi;
Mwenye uchungu natubu, Bwana narudi.
3
Nimechoka maovuni, sasa narudi;
Pendo lako lanivuta, Bwana narudi.
4
Ndilo tumaini langu, sasa narudi;
Yesu alinifilia, Bwana narudi.
5
Damu yake yanitosha, sasa narudi;
Unioshe kenyekenye, Bwana narudi.
- Title Nilipotoka Kabisa Key Titles undefined First Line Nilipotoka kabisa, sasa narudi; Author Year Composer Hymnal - Tune Metrical pattern # Stanzas Chorus Chorus Type Subjects Texts Print Texts Scripture Song