Advent Hymnals

107. SAUTI NI YAKE BWANA

Nyimbo Za Kristo,


1
Sauti ni yake Bwana, "Kwenda nani tayari?"
Mavuno yanakawia, Nani atayavuna?
Kwa kudumu anaita, Zawadi atatoa;
Nani atakayejibu, "Nipo Bwana nitume."

2
Kama huwezi safari, Hata nchi za mbali,
Pana watu karibuni, Wasiomjua Yesu;
Kama huwezi kusema, Jinsi ya malaika,
Waweza kuutangaza, Upendo wa Mwokozi.

3   
Ingawa huwezi kuwa, Mkesha mlangoni,
Ukiwatolea watu, Nafasi ya uzima;
Kwa sala na kwa sadaka, Watoa msaada,
Kama Harun mwaminifu, Kuinua mikono.

4
Roho za watu zikifa, Bwana akikuita,
Usiseme kwa uvivu, "Hakuna kazi kwangu".
Kwa furaha anza kazi, Ile aliyokupa,
Ukajibu mara moja, "Nipo Bwana nitume".



  • -
    Title Sauti Ni Yake Bwana
    Key
    Titles undefined
    First Line Sauti ni yake Bwana, “Kwenda nani tayari?”
    Author
    Year
    Composer
    Hymnal -
    Tune
    Metrical pattern
    # Stanzas
    Chorus
    Chorus Type
    Subjects
    Texts
    Print Texts
    Scripture Song