Advent Hymnals

106. HUNA KITU KWA YESU

Nyimbo Za Kristo,

1
Ukitafuta mali, Huna wasaa kwa Yesu?
Kwa matendo ya haki Huna wasaa kwa Yesu?
Anasa za dunia, Mambo yako ya raha
Haya unatafuta; Huna wasaa kwa Yesu? 

2
Mambo yanakusonga: Kwakehuna nafasi? 
Watekwa na dunia, Kwake huna nafasi?
Humwona m-langoni, Anapopiga hodi?
Daima hukusihi: Kwake huna nafasi? 

3
Sa-a ni za thamani, Kwake hamnayo kazi
Wala hamfanyi bidii, Kwake hamnayo kazi? 
Hamkufikia kwao Waliomo shimoni
Na waliopotea? Kwake hamnayo kazi? 

4
Na wazaa majani tu? Huna tunda kwa Yesu?
Mikono I mitupu, Huna tunda kwa Yesu?
Huna chembe kwa ghala Kazi yako kulipa; 
Wala huna furaha Unapomwona Yesu?



  • -
    Title Huna Kitu Kwa Yesu
    Key
    Titles undefined
    First Line Ukitafuta mali, Huna wasaa kwa Yesu?
    Author
    Year
    Composer
    Hymnal -
    Tune
    Metrical pattern
    # Stanzas
    Chorus
    Chorus Type
    Subjects
    Texts
    Print Texts
    Scripture Song