Advent Hymnals

091. KAA NAMI

Nyimbo Za Kristo,


1
Kaa nami, ni usiku tena;
Usiniache gizani, Bwana;
Msaada wako haukomi;
Nili peke yangu kaa nami.

2
Siku zetu hazikawi kwisha;
Sioni la kunifurahisha;
Hakuna ambacho hakikomi;
Usiye na mwiso, kaa nami.

3
Nina haja nawe kila saa;
Sina mwingine wa kunifaa;
Mimi nitaongozwa na nani
Ila wewe Bwana, kaa nami.

4
Sichi neno uwapo karibu;
Nipatalo lote si taabu;
Kifo na kaburi haviumi;
Nitashinda kwako kaa nami.

5
Nilalapo nikuone wewe,
Gizani mote nimulikiwe;
Nuru za mbinguni hazikomi;
Siku zangu zote kaa nami.



  • -
    Title Kaa Nami
    Key
    Titles undefined
    First Line Kaa nami, ni usiku tena;
    Author
    Year
    Composer
    Hymnal -
    Tune
    Metrical pattern
    # Stanzas
    Chorus
    Chorus Type
    Subjects
    Texts
    Print Texts
    Scripture Song